Sunderland ya msajili Moyes
Man U wakubali kumsajili Pogba kwa dau la Euro Mil 110
Man u imekubali kumsajili Paul Pogba kwa dau la kuvunja record ya dunia la Euro milion 110, Maafisa wa Man U wanatarajiwa kukutana na wawakilishi wa Juventus hapo jumatano kukamilisha huo uhamisho.
Pogba anatarajiwa kuvunja rekodi ya dunia kwa uhamisho kwa kumpita Gareth Bale aliyesajili na Real Madrid kutokea Tottenham kwa dau la Euro Million 100. Pogba anatarajiwa kulipwa Euro Million 13 kwa mwaka na amesema yupo tayari kufanya kazi na Man U.
TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE
Leicester City
wanataka pauni milioni 45 kumuuza Riyad Mahrez, 25, lakini wana uhakika kuwa
mchezaji huyo wa kimataifa wa Algeria atabakia King Power Stadium hasa baada ya
kuondoka kwa N'Golo Kante kwenda Chelsea (Telegraph), Manchester United
wamechelewesha kutangaza namba za jezi za wachezaji wake kwa msimu mpya mpaka
watakapokamilisha usajili wa pauni milioni 105 wa kiungo wa Ufaransa na
Juventus, Paul Pogba, 23 (Sun), mwenyekiti wa West Ham, David Sullivan, amesema
mshambuliaji Diafra Sakho, 26, haondoki labda timu hiyo ipate mchezaji
atakayeweza kuziba pengo lake (Mirror), Arsenal wanapanga kusajili wachezaji
wawili kwenye safu ya ulinzi, wakimtaka Jason Denayer, 21 kutoka Manchester
City na Matthias Ginter, 22 kutoka Borussia Dortmund (Sun), Bayern Munich na
Real Madrid bado wanamfuatilia winga anayesakwa na Manchester City, Leroy Sane,
20, kwa mujibu wa baba wa mchezaji huyo kutoka Ujerumani (Manchester Evening
News), dau la Arsenal la pauni milioni 2 limekubaliwa na Bolton la kumsajili
beki Rob Holding, 20 (Daily Mail), meneja wa Hull City, Steve Bruce, amekuwa
mtu wa pili kufanyiwa usaili wa kuwa meneja wa England, lakini anatarajiwa tu
kupewa kazi hiyo iwapo Sam Allardyce hatokubaliana na maslahi yaliyopo (Daily
Mail), Barcelona, Real Madrid, Manchester United na Chelsea zimepanda dau la
kumtaka kiungo kutoka Ureno anayecheza Valencia, Andre Gomes, 22, anayedhaniwa
kuwa na thamani ya pauni milioni 54 (Mundo Deportivo), Watford wanamfuatilia
beki kutoka Ivory Coast Brice Dja Djedje, 25, kutoka Marseille (L'Equipe),
Diego Costa, 27, hajaomba kuondoka Chelsea, na mshambuliaji huyo anatarajiwa
kusalia Darajani msimu ujao (Evening Standard), meneja wa Chelsea Antonio Conte
amekuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na mshambuliaji wa Real Madrid, Alvaro
Morata, 23, akimhakikishia nafasi yake iwapo ataamua kujiunga na Chelsea msimu
ujao (Marca), meneja wa Everton Ronald Koeman, anamfuatilia kiungo wa Ureno na
Sporting Lisbon William Carvalho, 24 (Mirror), Juventus wanakaribia kuwazidi
kete AC Milan katika kumsajili winga kutoka Croatia, Marko Pjaka, 21, ambaye tayari
ameaga wachezaji wenzake katika klabu ya Dinamo Zagreb (Gazzetta World),
mshambuliaji wa zamani wa Manchester City Alvaro Negredo, 30, hatosafiri na
timu yake ya Valencia kwenda Uholanzi, na badala yake atakwenda England kwa
ajili ya vipimo vya afya kabla ya kujiunga na Middlesbrough (Gazzetta Live),
Marseille wanafikiria kumchukua kwa mkopo mshambuliaji kutoka Cameroon,
anayechezea Tottenham, Clinton N'Jie, 22, iwapo winga wao Georges-Kevin
N'Koudou atakwenda White Hart Lane (Telegraph). Tetesi nyingine kesho
tukijaaliwa.


