Msichana wa miaka 17 mkazi wa Makete mkoani Njombe Vumilia Kyando ambaye
ni mhudumu wa baa amemnyonga na kumtumbukiza kwenye mto mtoto wake wa
kumzaa mwenye miaka miwili baada ya kupata mchumba ambaye si baba wa
mtoto huyo aliyetaka kuishi nae lakini akawa hataki kukaa na mtoto huyo.
Kamanda Podinsiana Protas amesema kuwa mwanamke huyo anahojiwa na polisi na upelezi ukikamilika atapelekwa Mahakamani.